Tafuta DHWTangazaTuandikie
Ni Safari ya Dunia - Matonya

Ikiwa ni zaidi ya miaka mi-nane tangu aingie rasmi katika gemu ya Bongofleva, msanii nyota wa kuimba nchini Matonya amekamilisha albam yake ya tatu inayoitwa `Safari ya Maisha`.

Ikibeba nyimbo 10, albam hiyo iliyoshirikisha wakali kadhaa wa muziki wa kizazi kipya, itaingia sokoni siku yoyote kuanzia sasa, anasema msanii.



``Ni bonge la albam,`` alisema Matonya kuzungumzia albam yake hiyo inayokuja sokoni.

``Kuna ma-ujumbe mazito, beat za hatari na featuring za nguvu.``

Alisema miongoni mwa nyimbo zilizomo na wasanii aliowashirikisha ni `Anita` ft Lady Jaydee, `Sina la Kufanya` ft TID, `Cum Back 2 Me` ft Joslin, `Tafadhali Njoo`, `Nishike Bega Langu`, `Tazama Macho Yangu` na uliobeba jina la albam wa `Safari ya Dunia` aliomshirikisha `Heavy Weight MC` Profesa Jay.

Mkali huyo kutoka mkoani Tanga amesema nyimbo za albam hiyo zimerekodiwa katika studio tofauti za hapa nchini na pia Nairobi Kenya.

``Wimbo wa `Anita` nimeurekodi kwa prodyuza Dunga na `Tafadhali Njoo` na `Nishike Bega Langu` nimezirekodi kwenye studio ya Zebra Records ya Kenya,`` alimalizia.


 Gonga hapa kutoa maoni yako kuhusu story hii...!!!
 Gonga hapa kusoma maoni hayo...!!!

 Mtumie Rafiki  Print nakala

 

Archive/Kumbukumbu:


Copyright © 2007 Darhotwire.com All rights reserved.Design by Infocomtechnologies Limited.