Wenye ndoto changamkieni tenda
Wabongo wametakiwa kujitokeza na mabizness ideas yatakayowezesha kujipatia mikopo ya kujiendeleza na kufuta umaskini.
Unachotakiwa kufanya ni kuibuka na mradi wako aidha mpya au wa namna ya kuendeleza uliopo katika mpango wa ushindani wa kibiashara -Tanzania Business Plan Competition.
Mpango huo umepewa kauli mbiu ya kimombo ya Believe, Begin, Become na uko chini ya Google.org ya Marekani, Techno Serve na M&M Communications.
Akizindua mpango huo Rais JK alisema kuwa wengi wenye ndoto zao zinazoweza kugeuzwa kuwa kweli endapo wangepatiwa mitaji, teknolojia na namna ya kusimamia miradi yao.
Aliwataka wengi kujitokeza kuchangamkia tenda hiyo katika kufuta umaskini kwa kupata ujuzi zaidi
kuboresha huduma na kupiga mzigo kwa nguvu katika kuhimili ushindani wa kibiashara.

Gonga hapa kutoa
maoni yako kuhusu story hii...!!!

Gonga hapa kusoma
maoni hayo...!!!
Mtumie Rafiki |
Print nakala