ufundishwaji wa kukariri unalemaza hesabu.
Ikiwa wanafunzi wataendelea kufundishwa somo la hisabati kwa kukariri kanuni, ongezeko la wengi kufeli na kutopenda somo hilo kutaendelea.
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mwantumu Mahiza,alitoa changamoto hiyo maadhimisho ya Siku ya Pai yaliyofanyika katika viwanja vya Taasisi ya Elimu, Mwenge Dar es Salaam.
Katika risala alisema wanafunzi wengi wamekuwa wakifeli somo hilo kutokana na mbinu zinazotumika kufundishia somo hilo ikiwemo kukariri.
Aliwataka walimu kubadilika kwa kuwashirikisha wanafunzi kuanzia katika utengenezaji wa dhana za kufundishia kwani njia hiyo itawapa urahisi wa kuelewa haraka.

Gonga hapa kutoa
maoni yako kuhusu story hii...!!!

Gonga hapa kusoma
maoni hayo...!!!
Mtumie Rafiki |
Print nakala