Mitandio inavyosevu maduu!!
Mitandio wazungu wanaita ’Scarf ’imechukua nafasi katika mavazi ya sasa ya wanawake hususan wadada wa kileo wanaoenda na wakati.
Mitandio hiyo ambayo iko ya aina tofauti mizito mepesi na ya rangi tofauti nayo ina matumizi tofauti kulingana na wakati na mazingira mvaaji aliyokuwepo.
Hapa bongo naona imeshachukua nafasi ya kanga na hata masweta kwani warembo wengi hutumia mitandio kujitanda kwenye baridi na wengine hujitanda kwenye misiba na haya kwenye sherehe mfano Kitchen Part.
Zaidi ya kutumika hivyo Scarf hujitanda kwa ajili ya show tu, mfano waweza valia sare na nguo ukajitanda shingoni au ukavaa scarf ambayo ina rangi zinazorandana na nguo, viatu au pochi katika tu ya kujiweka smart na mwenye mvuto zaidi.
Wapi waweza itundika......shingoni, mkononi ,ukajifunga kichwani au hata ukaegesha kiunoni, begani kokote upendapo ila inategemea na mazingira na ulivyovaa we mwenyewe na haijalishi kama umevaa gauni, skert au hata suruali ya kitambaa au jeans
ipo mingi ya rangi tofauti yenye chata za wabunifu maarufu hususan wale wanaodesign nguo za kike.
.....unaambiwa kama waogopa kuvaa rangi zaidi ya nyeupe na nyeusi basi vaa scarf yenye rangi kali kwani ni mojawappo ya kukutoa uoga na kuyafanya mavazi yako yawe bomba zaidi......we waonaje iyooooo
 |

Gonga hapa kutoa
maoni yako kuhusu story hii...!!!

Gonga hapa kusoma
maoni hayo...!!!
Mtumie Rafiki |
Print nakala