Tafuta DHWTangazaTuandikie
PEDICURE!!



Saloon nyingi za kisasa hazijakamilika bila kuwa na kitu kinaitwa pedicure na manicure ila leo naomba niwadokeze kuhusu pedicure

Pedicure maana halisi ni uoshaji wa miguu kuanzia unyayo hadi kucha

Zipo mashine maalum kwa ajili ya pedicure japokuwa wengine hutumia beseni tu kwa ajili ya shughuli hiyo pevu

Kienyeji unaweza chukua beseni ukaweka maji na sababu ile ya maji pamoja na dettol kidoogo kisha unaloweka miguu kwa nusu saa.....au unaweka ndani ya hilo machine ambayo inakuwa kama inavibrate na kusaidia kumassage unyayo.

Baada ya miguu kulainika ngozi inakuwa imeshalainika na unaanza kusugua kutoa dead skin(Kitaalam) hivyo inaondoa ile ngozi iliyojichokea, kisha unasugua kucha pamoja na kutoa vinyama vya pembeni ya kucha.

Ukipenda unachukua scrub unasugua miguu na kisha unaifuta na kuipaka lotion na kupaka rangi ya kucha kama mpenzi wa rangi.

Hapo unakuwa nadhifu kuvaa sandoz


Vifaa hivyo vinavyotakiwa kwenye pedicure


 Gonga hapa kutoa maoni yako kuhusu story hii...!!!
 Gonga hapa kusoma maoni hayo...!!!

 Mtumie Rafiki |   Print nakala

 

Archive/Kumbukumbu:


Copyright © 2007 Darhotwire.com All rights reserved.Design by Infocomtechnologies Limited.