Visura wa Tanzania waingia kambini!!
Wanamitindo 13 wanaoshiriki shindano la kisura wa Tanzania wameingia kambini kwa ajili ya kufanya stage ya pili ya shindano lao 'Face of Tanzania'
Akiongea na Darhotwire mratibu wa shindano hilo Irene kiwia alisema kuwa wanamitindo hao kutoka mikoa mbali mbali nchini wote wameshafika na wameingia kambini kwa ajili a kujifua na shindano hilo
'" shindano litafanika kwa muda wa
mwezi mmoja ambapo wasichana 3 watatolewa kambini na wasichana 10 watapanda jukwaani kuonesha mavazi ya wabunifu tofauti na mshindi kutajwa.
alisema wasichana hao wakiwa kambini watafundishwa na wataalam jinsi ya kupiga picha na mambo mbalimbali yahusuyo mitindo ambapo wadau watakuwa wanaona kupitia katika TV na msichana atakayeshindwa kwenda sambamba na maelekezo atakuwa anatolewa kwa kura za wadau
Haya kila la kheri

Gonga hapa kutoa
maoni yako kuhusu story hii...!!!

Gonga hapa kusoma
maoni hayo...!!!
Mtumie Rafiki |
Print nakala