Miss Tanzania wajazwa mapesa
Kampuni ya Simu za mkononi inayodhamini shindano la
Miss Tanzania ,Vodacom, limeongeza dau katika
udhamini wake wa mwaka huu
Akiongea jijini Meneja udhamini na Mawasiliano,
Ephraimu Mafuru alisema kuwa mwaka huu kampuni
yake itatumia sh.milioni 600 kudhamini shindano hilo
"Nia ya kuongeza zawadi ni kuyapa hadhi mashindano
haya ambayo wengine bado wanayachukulia ni uhuni na
kutaka wazazi wawaruhusu watoto wao washiriki kwa
wingi" alisema Mafuru.
Alisema udhamini huu utaanzia ngazi ya kitongoji na
kanda na kitaifa kama ilivyokuwa miaka iliyopita,Mwaka wa kwanza wa udhamini wa Vodacom walianza na mrembo Wema.
Haya warembo jinoeni mwaka wakutoka huo!!

Gonga hapa kutoa
maoni yako kuhusu story hii...!!!

Gonga hapa kusoma
maoni hayo...!!!
Mtumie Rafiki |
Print nakala