Tafuta DHWTangazaTuandikie
Mapishi ya firigisi za kuku


Mahitaji

Firigisi za kuku gramu 200, pilipili mboga moja, tangawizi gramu 5, pilipili manga gramu 2, vitunguu saumu gramu 5, mchuzi wa chaza gramu 5

Njia

1. chemsha maji, halafu weka firigisi ya kuku kwenye maji ya moto, halafu zipakue, na uziweke kwenye maji ya baridi. Kata firigiri ya kuku iwe vipande.

2. kata tangawizi, vitunguu saumu, pilipili mboga iwe vipande.

3. washa moto tia mafuta kwenye sufuria, tia vipande vya tangawizi, vitunguu saumu na pilipili manga kwenye sufuria, korogakoroga, tia firigisi za kuku kwenye sufuria, pilipili mboga, korogakoroga, mimina mchuzi wa chaza, korogakoroga. Mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.

Imeandaliwa na cri


 Gonga hapa kutoa maoni yako kuhusu story hii...!!!
 Gonga hapa kusoma maoni hayo...!!!

 Mtumie Rafiki |   Print nakala

 

Archive/Kumbukumbu:


Copyright © 2008 Darhotwire.com All rights reserved.Design by Infocomtechnologies Limited.