Tafuta DHWTangazaTuandikie
Mapishi ya kuku na limao




Mahitaji:

Nyama ya kuku gramu 300, wanga gramu 100, maji juisi ya limao gramu 250, sukari gramu 30, nyanya gramu 100, chumvi gramu 3, mvinyo wa kupikia gramu 5, vitunguu maji gramu 3, tangawizi gramu 3.

Njia:

1? Osha nyama ya kuku halafu uikate iwe vipande, koroga pamoja na chumvi, mvinyo wa kupikia, pilipili manga, tangawizi na vitunguu maji. Koroga maji juisi ya limao pamoja na unga, chumvi, pilipili manga, yai na mafuta.

2? Washa moto, mimina mafuta kwenye sufuria, weka vipande vya nyama ya kuku kwenye unga uliokorogwa, halafu weka ndani ya sufuria vikaange, halafu vipakue.

3? Washa moto tena, mimina maji kwenye sufuria, halafu tia chumvi, sukari, maji juisi ya limao, korogakoroga halafu mimina maji ya wanga, korogakoroga, tia vipande vya nyama ya kuku korogakoroga vipakue. Mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.

Imeandaliwa na CRI



 Gonga hapa kutoa maoni yako kuhusu story hii...!!!
 Gonga hapa kusoma maoni hayo...!!!

 Mtumie Rafiki |   Print nakala

 

Archive/Kumbukumbu:


Copyright © 2008 Darhotwire.com All rights reserved.Design by Infocomtechnologies Limited.