Kolelo kuzinduliwa leo
Ni filamu iliyotungwa na mwanadada Irene Sanga mtunzi wa kile kibao cha Salamu zako Mjomba kilichomtoa Mrisho Mpoto
Irene ambaye ni mwanamuziki wa bendi ya Parapanda Arts amesema filamu hiyo imetengenezwa katika mazingira ya kitanzania na wasanii wakongwe katika fani, itazinduliwa leo katika ukumbi wa Dar West Tabata na kusindikizwa na bendi ya FM Academia
...filamu hiyo ambayo imetengenezea katika mlima wa Kolelo zaidi ya kutengenezwa na wakongwe pia inasisimua, inahuzinisha na kufurahisha pia
Waigizaji hao wanaounda filamu hii ni pamoja na Fundi Said maarufu kama Mzee Kipara, Riyama Ally,Tekla Mjata na kuongozwa na Hammie Rajab
Filamu hiyo inazungumzia habari ya ukweli inayohusu mzimu unaoishi kwenye mlima huo tangu karne ya 19 hadi sasa. ambao uliandikwa katika kitabu cha maajabu ya Mlima Kolelo kilichoandikwa na Hammie Rajab

Gonga hapa kutoa
maoni yako kuhusu story hii...!!!

Gonga hapa kusoma
maoni hayo...!!!
Mtumie Rafiki |
Print nakala