Tafuta DHWTangazaTuandikie
Mapishi ya nyama ya ng'ombe na njegere


Mahitaji

Nyama ya ng'ombe gramu 300, karoti moja, njegere gramu 150, vipande vya vitunguu maji,, tangawizi na vitunguu saumu kila kijiko kimoja, chumvi kijiko kimoja, mchuzi wa sosi vijiko viwili, sukari vijiko viwili, siki vijiko viwili, maji ya wanga vijiko vitano.

Njia

1. osha nyama ya ng'ombe, halafu uikate iwe vipande vidogovidogo, ondoa maganda ya karoti halafu uikate iwe vipande vidogovidogo.

2. washa moto tia mafuta kwenye sufuria, mpaka yawe na joto la nyuzi 60, tia njegere, kaanga, halafu zipakue.

3. washa moto tena, tia vipande vya vitunguu maji, tangawizi na vitunguu saumu kwenye sufuria korogakoroga, tia vipande vya nyama ya ng'ombe, korogakoroga, halafu tia vipande vya karoti, korogakoroga, tia sukari, siki, mchuzi wa sosi, chumvi, korogakoroga, mimina maji ya wanga, korogakoroga tia njegere korogakoroga, ipakue. Mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.

Imeandaliwa na CRI



 Gonga hapa kutoa maoni yako kuhusu story hii...!!!
 Gonga hapa kusoma maoni hayo...!!!

 Mtumie Rafiki |   Print nakala

 

Archive/Kumbukumbu:


Copyright © 2008 Darhotwire.com All rights reserved.Design by Infocomtechnologies Limited.