Tafuta DHWTangazaTuandikie
Pale za comedy wanapotoa 'chorus'


Vijimsema kibao pamoja na vitendo vya kundi la Ze comedy vimeenea mitaani kama sio Bongo nzima kiasi cha kupelekea kmakundi mbalimbali ya muziki nchini kupata cha kuimba au kunogeshea miziki yao

Hayo nimeyathibitisha kupitia nyimbo ya mama wa mipasho maarufu jijini kama Khadija Kopa katika wimbo wake mpya wa Why?!!

Katika wimbo huo kuna kiitikio kinasema Why?!!...kwanini...endeleaaaa...Hayo yakiwa ni maneno ambayo yanapendwa kusemwa na mchekeshaji Mac Regan

Kama hiyo haitoshi nalo kundi la Jahazi Modern Taarab wana nakshi nakshi wana kichombezo chao katika sebene zao kinachosema...cheza kijot jot na kushtua...huku style ya kucheza ikiwa ni ile ya mwendo atembeao Jotti katika michezo yao ya kila alhamis ndani ya Runinga ya EATV

Ukiachia mbali misemo kama Mdebwedo, kugandamiza, mwanawane, namengine kibao imeenea mitaani ambayo hutoka katika vinywa vya wachekeshaji hao.

Na huo ni mwanzo!!


 Gonga hapa kutoa maoni yako kuhusu story hii...!!!
 Gonga hapa kusoma maoni hayo...!!!

 Mtumie Rafiki |   Print nakala

 

Archive/Kumbukumbu:


Copyright © 2008 Darhotwire.com All rights reserved.Design by Infocomtechnologies Limited.