Tafuta DHWTangazaTuandikie
Tetesi zimezagaa



mastaa wa filam Tanzania wamedhulumiwa haki yao na kampuni moja inayojulikana kwa jina la Billionaire Club(Escape)

Kwa mujibu wa mtandao wa Ray Kampuni hiyo iliwaahidi mastaa hao kuwalipa malipo mazuri na ahadi kemkem kwa minajili ya kufanya nao kazi za kutengeneza filam na Tamthilia kwa kuingia nao mikataba ya miezi sita ,badala yake wasanii hao walifaidi mkataba wao kwa muda wa mwezi mmoja na baada ya hapo hali ikawa tofauti na mkataba unavyosema na wamiliki wa kampuni hiyo kuanza kuwakimbia wasanii hao.

Sakata hili limeibuka baada ya msanii Vanita Omary ambaye anajishughulisha na make up na costume kupelekwa polisi na mmoja wa mabosi wa kampuni hiyo baada ya kukataa kurudisha costume za kampuni hiyo mpaka watakapolipwa haki zao ndio warudishe

Wasanii ambao wako kwenye mkumbo huo ni Yusuph Mlela,Monalisa,Thea,Big Matovolwa,Rose Ndauka,Vanita Omary,Frank Mwikongi

Kipindi cha Bongo Movie kimeteta nao...tusubiri luningani EATV .



 Gonga hapa kutoa maoni yako kuhusu story hii...!!!
 Gonga hapa kusoma maoni hayo...!!!

 Mtumie Rafiki |   Print nakala

 

Archive/Kumbukumbu:


Copyright © 2010 Darhotwire.com All rights reserved.Design by Infocomtechnologies Limited.