Mengi yamekuwa yakisemwa kuhusu kupanda na kushuka kwa uchumi wa taifa hili, ilihali wananchi pamoja na juhudi zao zote za kujitafutia maendeleo wamekuwa hawauoni moja kwa moja uchumi huo mifukoni mwao. Je nini maana ya kupanda kwa uchumi kwa mwananchi wa kawaida

Share |

UCHUMI UNAOKUA LAZIMA UPUNGUZE UMASIKINI KATIKA JAMII

MACHWA

Tangu uhuru wa Tanganyika kweli kuna baadhi ya mambo ambayo tulipiga hatua nzuri kiasi kwa vipindi flani tu kama lakini baadaye mambo yakawa tofauti sana hasa baada ya mkutano uliofanyika Zanziba ambao ulionesha kuwa maamuzi yake ylifuta baadhi ya maazimio ya azimio la arusha. Ukiangalia kwa undani njia kuu za uchumi hazipo mikononi mwa wananchi tena. Tunaambiwa uchumi unakua kila mwaka lakini anagalia masikini wanaongezeka kiasi gani.Kwa kuwa uchumi mzuri ni ule unaopunguza umasikini kwenye jamii. Angalia gap kati ya maskini na matajiri ni kubwa kiasi gani.